Askari wawili wafariki Dunia mkoani Mbeya


Gari aina ya Landrover mali ya Jeshi la Polisi kikosi cha kutuliza ghasia mkoa wa Mbeya yenye no PT.2079 likiendeshwa na askari no. G.3452 PC Adam miaka 30, iliacha njia na kupinduka wakati  linawapeleka askari kazini leo Alhamisi january18. 2018 majira ya saa kumi na dakika 45 jion maeneo ya Iwambi barabara ya Mbeya Tunduma kata ya Iwambi tarafa ya Iyunga jiji na Mkoa wa Mbeya na kusababisha vifo vya askari wawili ambao ni
H.1215PC Prosper s/o Jordan Chalamila miaka 29, wa FFU Mbeya na

1.   H.4335 PC Mathew s/o Jailos Mpogole miaka 26, wa FFU Mbeya

Na Kujeruhi askari wengine 9 ambapo kati yao watatu wamelazwa katika hospitali ya rufaa Mbeya;
1.   G.3452 PC Adam miaka 30, ambaye ameumia maeneo ya kifua
2.   G.6849 PC Khamis Ally miaka 32, ambaye ameumia maeneo ya kichwani.
3.   H. 6952 PC Kelvin s/o Martini miaka 28, ambaye ameumia maeneo ya kichwani/ usoni
Askari wengine 06, Walitibiwa na kuruhusiwa ambao ni;
1.   H.3929 PC Leonard Michael miaka 26, Alipata jeraha mkono wa kushoto.
2.   H.469 PC Fredy Mbande miaka 28, alipata jeraha mgongoni.
3.   H.948 PC David Ibrahim miaka 27, alipata maumivu ya mwili.
4.   G.9588 PC Marwa Itembe miaka 29, Alipata maumivu ya mwili.
5.   H.1325 PC Christopher Daniel Msangi miaka 26, alipata maumivu ya mbavu.
6.   H.6789 PC Lucas Andrea Mashala miaka 24, ambaye alipata jeraha kichwani kulia na maumivu ya mbavu kulia.

Miili ya marehemu imehifadhiwa katika hospitali ya rufaa Mbeya huku Chanzo cha ajali kikitajwa kuwa ni mwendo kasi

No comments