CAG yabaini madudu katika halmashauri ya jiji la Tanga
TANGA
Kamati ya bunge ya hesabu za serikali za mitaa nchini imebaini uwepo wa madudu mengi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya halmashauri ya jiji la TANGA huku kamati hiyo ikitoa maagizo mazito kwa halmashauri ya jiji la Tanga.
Kamati ya bunge ya hesabu za serikali za mitaa nchini imebaini uwepo wa madudu mengi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya halmashauri ya jiji la TANGA huku kamati hiyo ikitoa maagizo mazito kwa halmashauri ya jiji la Tanga.
Miongoni mwa madudu hayo ni uwepo wa
suala la ukosefu wa uratibu,uandaaji sanjari na usimamizi bora wa miradi ya
halmashauri kwa muda mrefu.
Nyengine ni kutokua na ushirikishwaji wa
vijana katika utekelezaji wa miradi mingi ya uwekezaji jambo ambalo linawanyima
fursa vijana ya kutambua fursa za kazi zitokanazo na uwekezaji husika katika
halmashauri hiyo.
Hayo yamebainika katika ziara ya kamati
hiyo walioifanya jijini Tanga juu ya kuitembelea miradi mbalimbali ya
maendeleo.
Akizungumza kwa niaba ya kamati hiyo
mbele ya waandishi wa habari,viongozi wa halmashauri ya jiji,viongozi wa wilaya
sanjari na mkoa kwa ujumla,Mwenyekiti wa kamati hiyo Mheshimiwa ABDALLAH
CHIKOTA amesema mbali na kubaini hayo pia wamebaini uwepo wa taarifa
zinazokinzana za watendaji wa halmashauri juu ya utekelezaji wa miradi ya
kimaendeleo katika halmashauri hiyo.
Mhe.Chikota amesema miongoni mwa miradi
walioigundua uwepo wa kasoro hizo ni mradi wa maji katika kijiji cha mwarongo
kata ya MARUNGU uliogharimu shilingi milioni 622.9 ambao umekua ukisuaua
kuwahudumia wananchi wa maeneo husika kutokana na kupasuka kwa mabomba ya mradi
huo.
Mradi mwengine ni ule wa milioni 280.6
wa soko la mgandini liliopo kata ya MWANZANGE ambao umegubikwa na dosari lukuki
ikiwa ubovu wa miundombinu ya soko, ukosefu wa uzio,maji,umeme ,baadhi ya
maeneo ya soko kuvuja sanjari na ukosefu wa hali ya ushirikishwaji na
mawasiliano mazuri kati ya wafanyabiashara wa soko hilo na uongozi wa
halmashauri jambo ambalo huleta mgongano wa mara kwa mara baina yao.
Katika hatua nyengine mwenyekiti huyo
ametoa maagizo ya kamati hiyo ambapo imeuagiza uongozi wa halamashauri hiyo
kutekeleza kwa vitendo suala la kisheria ya kutoa asilimia kumi ya vijana na
wakinamama katika halmashauri hiyo kwa kuwa kumebainika sheria hiyo haifuatwi
ipasavyo katika halmashauri hiyo.
Halikadhalika kamati hiyo imepiga
mafuruku tabia ya viongozi wa halmashauri hiyo kuingia mikataba ambayo haina
masilahi katika taifa kwa kuwakodisha wawekezaji ardhi na huku kamati hiyo ikiiagiza
halmashauri ya jiji kutoingia mkataba wa aina yeyote ile na wawekezaji hadi
jopo la viongozi wa mkoa,wizara husika itakapo kaa na kujiridhisha kuhusu tija
ya mkataba husika katika halmashauri.
Pia kamati imeuagiza uongozi wa
halmashauri ya jiji la Tanga kuzifanyia utatuzi changamoto zote zilizobainika
katika miradi hiyo ambapo hadi ifikapo April 28 mwaka huu taarifa ya
utekelezaji wake iwe imekwishawasilishwa katika ofisi za CAG na nakala ipelekwe
katika kamati hiyo.
Kwa upande wao katibu tawala mkoa wa
Tanga,Mhandisi.ZENA SAID,mkuu wa wilaya ya Tanga,THOBIAS MWILAPWA,Mstahiki meya
wa jiji la TANGA Mhe.SELEBOSS MUSTAPH MHINA pamoja na mkurugenzi wa jiji la Tanga DAUDI
MAYEJI,wameipongeza kamati hiyo kwa ziara walioifanya na huku wakiahidi
kutekeleza agizo hilo mapema iwezekanavyo.
Post a Comment