Licha ya Rais maguful kupiga stop michago mashuleni bado korogwe vijijini wachangishwa kila mzazi 53,600


KOROGWE.
Wananchi wa Tarafa ya MAGOMA,halmashauri ya KOROGWE vijijini mkoani TANGA,wamepaza sauti zao kwa kuiomba serekali kuwasaidia kuweza kurudishiwa fedha zao walizochangishwa kwaajili ya watoto wao waliojiunga na kidato cha kwanza.

Mapema wakizungumza na MAJLIS MEDIA   hii leo kwa hisia kali wananchi kutoka maeneo ya MAGOMA,MASHEWA na FOLOFOLO,wameanza kwa kutoa shukuran kwa mheshimiwa Rais magufuli kupiga marufuku michango mashuleni, na kuongeza kwamba licha ya marufuku hiyo lakini katika tarafa yao wamekwishachangishwa fedha kwaajili ya utengenezaji wa madawati ambapo wamedai kuwa kwa kila mzazi wa mtoto wa kidato cha kwanza ametoa shilingi 31,000 na wengine elfu 53,600.

Aidha,wamesema kuwa kutokana na maisha kuwa magumu kwa upande wao sasa ni wakati wakuweza kurudishiwa fedha hizo ili waweze kumudu gharama za maisha kwenye kaya zao wanazoishi.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya folo folo ABDALLAH HASSANI MDOE amekiri wananchi wake kuchangishwa michango hiyo kutokana na changamoto ya upungufu wa madawati katika shule ya sekondari ndani ya tarafa hiyo.

Awali,MJLIS MEDIA imelazimika kumtafuta mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Korogwe Vijijini Ndugu.GEORGE JOHN NYARONGA,ambapo kwa upande wake amesema kwamba ofisi yake haijatoa kibali chochote cha mzazi kuchangishwa michango mashuleni huku akiahidi kulifuatilia suala hilo kujua undani wake.

Halikadhalika Ndugu.GEORGE  NYARONGA amewatahadharisha watumishi wa masula ya elimu katika halmashauri hiyo kufanya kazi kwa uandilifu kwa kutojiusisha na masuala ya ujanja ujanja sanjari na uongo katika nyazifa zao hili waweze kujipatia fedha kwa kuwa hil ni kosa kisheria na maadili ya utumishi bora.





No comments