Mamia ya wananchi Tanga wafurika misikitini

Makundi kwa makundi ya wananchi wa halmashauri ya jiji la tanga,hii leo wamefurika katika misikiti mbalimbali iliopo jijini hapa kwaajili ya kuweza kujipatia huduma ya maji katika misikiti hiyo.

Mwanahabari mwandamizi wa majlis media ameyabainisha hayo wakati aliopofanya ziara endelevu ya ufuatiliaji wa hali ya huduma ya maji katika jiji la tanga. 

Hayo yamejitokeza kufuatia jiji la tanga kukumbwa na tatizo la ukosefu wa huduma ya maji safi na salama kutoka kwa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira tanga uwasa toka mwezi january kuanza mwaka huu

Miongoni mwa maeneo ya misikiti iliotembelewa na mwanahabari wa majlis leo na kukuta makundi ya wananchi wakifuata huduma hiyo ya maji ni msikiti wa Ibadhi bara bara ya 12,mabawa,shamsil maarif islamiya duga,msikiti wa mchuzi wa nyoka,magomeni na mingineo.

Wakizungumza na mwanahabari wa majlis media wananchi hao ambapo asilimia kubwa ni wakinamama wamesema kwamba wanapata adha lukuki katika kaya zao kutokana na ukosefu wa huduma hiyo muhimu katika maisha ya binadamu.  

Aidha,wametaja athari zilizojitokeza katika kaya zao kutokana na tatizo la ukosefu wa maji kuwa ni kushindwa kufanya kazi za uchumi kutokana kutumia muda mwingi kutafuta huduma ya maji,kutumia gharama kubwa kununua maji ya dukani kwaajili ya mahitaji ya nyumbani,kuumwa homa za matumbo kutokana na kutumia maji ambayo si salama kutoka visimani. 

Awali wananchi hao wameiomba serekali kupitia wizara ya maji na umwagiliaji kuboresha huduma za upatikanaji maji kwa kua hivi sasa mamlaka hiyo imezidiwa na wateja wa huduma hiyo hali inayosababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi.


No comments