Milioni 60 kumwagwa korogwe mji.
Halmashauri ya MJI KOROGWE mkoani TANGA,imedhamiria kutoa shilingi milioni 60 kwa wananchi wa
halmashauri hiyo ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Akizungumza na MAJLISI MEDIA
hii leo Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Ndugu.JUMANNE SHAURI amesema
fedha hizo wazitarajia kuzitoa ndani ya mwaka huu 2018 ambapo ni mwendelezo wa utoaji
wa asilimia kumi ya mapato ya ndani ya halmashauri kwa ajili ya vijana na wakinamama.
Aidha,amesema kwa kipindi
cha mwaka jana pekee walitoa shilingi milioni 40 kwa walengwa hao na sasa wanajishughulisha katika vikundi hai vya ujasiriamali na
biashara ndogo ndogo ikiwemo utengenezaji wa viatu sambamba na kujishughulisha
na usafiri wa bodaboda.
Mkurugenzi huyo amesema
walengwa hao wanawezeshwa nyenzo za biashara na si pesa tasilimu kama watu
wengine wanavyodhani na tayari jopo la wataalumu wa ujasiriamali kutoka
SIDO,maafisa ugavi na maafisa biashara wanaendelea na zoezi la utoaji elimu kwa
walengwa ili waweze kuisimamia mitaji yao vizuri.
Kwa upande wao baadhi ya
wajasiriamali walionufaika na asilimia hiyo mwaka jana wameipongeza halmashauri
hiyo kwa kuwakumbuka na kuahidi kuitumia kwa matumizi chanya mitaji mingine
watakayopatiwa mwaka huu.
Katika hatua nyengine
mkurugenzi JUMANNE SHAURI ameizungumzia mipango mikakati walionayo katika
halmashauri ni ujenzi wa soko kubwa la kisasa katika halmashauri ambapo ujenzi
huo unatarajia kuaanza mwezi wa pili mwaka huu,ujenzi wa Viwanda vidogo vidogo
ikiwemo kiwanda cha viatu,mkonge,kujenga kiwanda cha usindikaji matunda katika
halmashauri na pia tayari wametenga zaidi ya ekari 4000 kwaajili ya wawekezaji
mbalimbali katika halmashauri.
Awali amelizungumzia
suala la ukusanyaji wa mapato ya ndani ya halmashauri ambapo amesema asilimia
30 ya mapato ya halmshauri hutokana na stendi mpya ya kisasa iliopo katika halmashauri
hiyo ambayo kwa siku hukusanya zaidi ya milioni moja.
Halikadhalika amewaomba
wananchi wa halmashauri hiyo kuwa na mwitikio katika suala la kuitumia stendi
hiyo ili kuiwezesha halmashauri iweze kufanikisha adhima ya serekali ya kufikia
uchumi wa kati katika suala la ukusanyaji wa mapato ambapo amesema kuna baadhi
ya wananchi hawaitumii ipasavyo stend hiyo na kusubiri usafiri barabarani jambo
ambalo amesema linarudisha nyuma jitihada za ukusanyaji wa mapato kwa wingi katika
stend hiyo.
Post a Comment