RPC TANGA,Zoezi La Ukaguzi Wa Magari Ni Endelevu


Jeshi la polis mkoani TANGA,limesema zoezi la ukaguzi wa magari mbalimbali  mkoani hapa ni endelevu huku ikielezwa kwamba lengo kubwa la zoezi hilo ni kuweza kubaini uwepo wa vyombo vya moto vinavyokiuka sheria na kanuni za usafiri.

Maneno hayo yamesemwa hii leo na kamanda wa jeshi la polis mkoa wa TANGA,kamishina msaidizi mwandamizi wa jeshi,SACP.EDUARD BUKOMBE alipokua
akifanyiwa mahujiano mahsusi na mwanahabari wa MAJLIS MEDIA ofisini kwake.

Aidha,BUKOMBE amesema kuwa mwishoni mwa mwaka jana (2017) walifanikiwa kufanya kaguzi za mara kwa mara katika magari mbalimbali na kubaini uwepo wa tatizo kubwa la matumizi mabaya ya vyombo vya usafiri barabarani sambamba na uwepo wa magari mabovu ambapo amesema agenda hiyo ni endelevu na hivi sasa amekwisha liagiza jopo la wakaguzi waliobwebwea kuendelea na zoezi hilo mkoani hapa.

Katika hatua nyengine kamanda huyo ametoa onyo kwa wamiliki wa magari,madereva sambamba na wananchi kwa ujumla kufuata sheria za usalama barabarani na kusema katika uongozi wake hatomfumbia macho mtu yeyote anaekiuka sheria hizo.

Awali,Kamanda BUKOMBE amezungumzia suala la utendaji kazi wa vituo vya polis mkoani Tanga ambapo amesema utendaji ni mzuri na kuongeza kuwa mikakati aliyonayo kwa sasa ni kutengeneza mfumo mzuri kati ya wananchi na jeshi la polis kwa lengo la kutokomeza kabisa malalamiko yanayotolewa na wananchi dhidi ya wahudumu wa jeshi hilo katika vituo hivyo.


Pia amesema anatarajia kufanya ziara za mara kwa mara katika vituo vyote vya polis ili aweze kubaini uwepo wa askari wa jeshi hilo ambao si waadilifu katika majukumu yao na kutoa rai kwa askari wa jeshi polisi mkoani hapa kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya utumishi bora wa viongozi wa umma nchini.

No comments