Ukosefu wa damu katika hospital ya bombo wafika mwisho

Mratibu wa huduma za maabara mkoa wa TANGA,MUSSA JUMA KAYANDA akiongea mwandishi wa MAJLIS MEDIA mapema leo
Hospital ya rufaa ya mkoa wa TANGA BOMBO inatarajia kuanzisha mpango kabambwe wa kuhakikisha huduma ya upatikanaji wa damu salama katika hospital zote za serekali mkoani hapa inaimarika kwa kiwango kikubwa zaidi.
Aidha,mpango huo ni kuvishirikisha zaidi vituo binafsi vya afya na kwa kila kituo kitaratibu zoezi la uchangiaji wa damu kwa kila mwezi kwa lengo la kupata Uniti 200 za damu huku mpango huo ukitarajiwa kuanza ndani ya mwezi huu january.
Mratibu wa huduma za maabara mkoa wa TANGA,MUSSA JUMA KAYANDA ameyasema hayo hii leo wakati alipokua akizungumza mubashara na MAJLIS MEDIA kuhusu hali halisi ya upatikanaji wa huduma hiyo damu salama mkoani hapa.

Awali,akiielezea hali halisi ya bank ya damu katika mkoa wa Tanga amesema mpaka sasa jumla ya unit 312 zipo katika banki hiyo na  zinatarajiwa kutumika kwa kipindi cha wiki mbili zijazo ndani ya mwezi huu ambao kwamchanganuao wilaya ya Pangani ina unit 26,Muheza unit 29,Handeni unit 57,Lushoto unit 10,Kilindi unit 31,Korogwe unit 42 na katika hospital ya bombo unit 125.

Mapema akitaja changamoto zinazoikabili sekta hiyo katika mkoa wa Tanga MUSSA KAYANDA amesema kuwa ni ukosefu wa kituo maalumu  cha uchangiaji wa damu salama katika mkoa  ambapo hivi sasa wapo mbioni kujenga kituo nje ya hospital ya bombo kitakachowezesha kutatua changamoto hiyo huku akiwashukuru wananchi wanaoendelea kushiriki katika zoezi la uchangiaji wa damu katika hospital hiyo na kutoa wito kwa wengine kuunga mkono zoezi la uchangiaji wa damu katika hospital za serekali kwenye maeneo yao.

Mratibu huyo amesema kwa kawaida kwa kila siku hospital za serekali katika mkoa wa Tanga kwa ujumla zinatumia unit 25 mpaka 30 za damu salama ambapo hospital ya bombo ikitajwa kuongoza kwa matumizi makubwa ya damu kwa kutumia unit 10 na ikifuatiwa na wilaya ya Muheza sanjari na Lushoto.

Halikadhalika amewatoa hofu wananchi wa mkoa wa TANGA kwa kusema kwamba hali ya upatikanaji wa damu salama katika hospital za serekali kimkoa zipo za kutosha, na katika hatua nyengine amesema tegemezi kubwa la  ukusanyaji wa damu hizo ni hospital ya rufaa ya mkoa huu bombo.
                           






No comments