Wananchi TANGA watakiwa kujiunga na NHIF.


Wananchi mkoani TANGA wametakiwa kujiunga na mfuko wa taifa wa bima ya afya (NHIF) ili kuondokana na changamoto ya ukosefu wa matibabu bora katika vituo vya afya.

Pia wametakiwa kuwasajili watoto wao wenye umri kuanzia siku moja mpaka kumi na minane katika mfuko wa bima ya afya wa toto afya kadi.
Bwana,ALY MWAKABABU ni meneja wa NHIF mkoa wa TANGA,ametoa wito huo hii leo wakati alipokua akifanyiwa mahujiano mahsusi na mwahabari wa MAJLIS MEDIA ofisini kwake.

Akizungumzia suala la mfuko wa toto afya kadi MWAKABABU amesema jambo hilo ni agenda yao kubwa kwa sasa kimkoa ambapo wanaendelea na uwamasishaji kwa wananchi ili waweze kukimbilia fursa hiyo na kuongeza kuwa lengo kubwa la serikali kuleta mfuko huo ni kuwasaidia wazazi ama  walezi unafuu wa kumudu gharama za matibabu kwa watoto wao pindi wanapougua maradhi mbalimbali.
  
Amesema kuwa mpaka sasa jumla ya idadi ya watoto waliosajiliwa katika mfuko huo hawafiki hata mia tano kimkoa ambapo amesema ni idadi ndogo sana  ukilinganisha na wingi wa wananchi waliopo katika mkoa mzima wa tanga.
Aidha,Mwakababu amesema kwamba ukosefu wa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa bima ya afya ni miongoni mwa changamoto iliyopelekea mkoa wa Tanga kuwa na idadi ndogo ya watoto waliosajiliwa katika mfuko huo ambapo amesema hivi sasa wanaendelea na ziara mbalimbali katika wilaya zote zilizopo mkoani hapa kwa lengo la kuwaelimisha wananchi umuhimu wa suala hilo.

Halikadhalika,amewaomba wajasiliamali wadogo wadogo mkoani Tanga kujiunga vikundi ili waweze kujisajili katika mfuko wa taifa wa bima ya afya NHIF katika biashara zao ili waweze kuinusuru mitaji yao isiweze kufa kutokana na kutumia gharama kubwa za matibabu pindi waendapo katika zahanati ama vituo vya afya.


Awali,meneja huyo wa bima ya afya mkoa wa Tanga ametumia fursa hii kwa kupaza sauti yake kwa kuwaomba waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari mkoani Tanga,kuisaidia serikali kuielimisha jamii kupitia vyombo vyao juu ya umuhimu wa bima ya afya katika kaya zao wanazoishi.

No comments