JESHI LA POLISI MKOANI TANGA,LIMEKUSANYA BILIONI TISA

Jeshi la polisi mkoani TANGA,limekusanya Bilioni 9,238,6,27,000 kutokana na makosa ya usalama barabarani kwa mwaka 2017 mkoani hapa.
majlismedia.blogespot.com
Akizungumza hii leo katika maadhimisho ya siku ya usalama barabarani kimkoa katika viwanja vya tangamano jijini hapa,mkuu wa kikosi cha usalalma barabarani mkoa wa TANGA,RTO SADIK RAMADHAN MSANGI amesema fedha hizo zinatokana na ukamataji wa makosa kuanzia kipindi cha januari mpaka November ambapo walifanikiwa kukamata makosa 39,860 na makosa 36,511 yalitozwa faini ya papo kwa papo na kupelekea ukusanyaji wa fedha hizo.

Amesema takwimu zinaonyesha kwamba mwaka 2017  makosa yamezidi ukilinganisha na mwaka uliopita wa 2016 ambapo kwa kipindi hicho  cha January mpaka November yalikua makosa 35,444,na makosa 32,235  yalitozwa faidi za papo hapo na kufanikiwa kukusanya kiasi cha pesa Milioni 975,8,20,000.

Aidha,amesema kwa upande wa  ajali za barabarani kwa mwaka huu 2017 zimepungua kutoka ajali 91 mwaka jana hadi ajali 70 mwaka huu,ambapo ajali zilizosababisha vifo kwa mwaka 2016 zilikua 67 na mwaka 2017 zilikua 53 na kusababisha vifo vya watu 86 kwa mwaka 2016 na watu 59 mwaka 2017,na kwa upande wa majeruhi kwa mwaka 2016 walikua 170,na 2017 walikua 112.

MSANGI ametaja mikakati mathubuti  juu ya  kuzithibitia ajali hizo kuwa ni kuongeza jitihada za kutoa elimu mashuleni na kwa madereva wa vyombo vya moto sanjari na kuongeza jitihada katika usimamizi wa sheria za usalama barabarani katika mkoa.

Awali mgeni rasmi wa maadhimisho hayo ambae ni kaimu mkuu wa mkoa wa tanga,ambae ni mkuu wa wilaya ya muheza mkoani hapa,Mhandisi.MWANAASHA RAJABU TUMBO amewapongeza askari wa jeshi la polisi katika usimamizi wa sheria za usalama barabarani huku akiwataka kuongeza juhudi katika kukemea vikali madereva wazembe wanaoendesha usafiri  wakiwa wamelewa.





No comments