Naibu wazir wa maliasili na utalii awaagiza wakuu wote wa wilaya kupanda miti milioni 1.5 katika kila wilaya

Naibu wazir wa maliasili na utalii ,mheshimiwa japhet hasunga amewaagiza wakuu wote wa wilaya nchini
kuhakisha wilaya zao zinapanda miti milioni 1.5  kwa vitendo kama sheria inavyoelekeza na si ubabaishaji.

Mheshimiwa hasunga ametoa kauli hiyo alipokua akizungumza kwa njia ya simu na mwanahabari wa radio nuur fm hii leo.

Amesema sheria inaelekeza kwa kila wilaya iweze kupatanda miti milioni 1.5 kwa kila mwaka lakini asilimia kubwa za wilaya zimekua zikikiuka sheria kwa kufanya ubabaishaji mkubwa ambapo wanaonyeshamiti walioipanda katika   makaratasi na si kiuhalisia wa miti yenyewe iliyopandwa.

Aidha,amesemaendapo miti hiyo itapandwa katika kila wilaya kutapunguza wimbi kubwa linaloonekana sasa la uharibifu wa misitu ya asili kwenye maeneo mbalimbali nchini. 

Katika hatua nyengine mheshimiwa naibu waziri huyo wa maliasili na utalii amesema kutokana na hivi sasa asilimia kubwa ya misitu kutotoa mapato stahiki katika nchi,serikali imejipanga kuanzisha viwanda vitakavyotegemea malighafi za misitu,kuandaa mpango kabambe wa utoaji vibali vya kusafirisha malighafi za misitu nje ya nchi ili sekta hiyo iwe tegemezi katika kuliingizia taifa mapato

 Amemaliza kwa kuwataka wananchi kutofanya uvamizi na uharibifu katika hifadhi ama misitu ya asili na badalayake wawe mfano wa kuigwa katika kuitunza misitu hiyo katika maeno yao wanayoishi.

No comments