Huduma ya maji safi jiji TANGA pasua kichwa

Hali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika halmashauri ya jiji la TANGA,imeanza kuadimika hali inayosababisha adha kubwa kwa wananchi kutokana na  ukosefu wa huduma hiyo.

MAJLIS MEDIA imebainisha hayo hii leo wakati ilipofanya ziara kwa nyakati tofauti katika kata za MSAMBWENI,MABAWA,DUGA,MAGAONI,TANGASISI,
MNYANJANI sambamba  na MASIWANI zilizopo jijini Tanga na kujionea hali halisi ya huduma hiyo ikisuasua kutoka kwenye vizimba vya maji.

Mapema wakizungumza na  MAJLIS MEDIA baadhi ya wananchi wa kata hizo wamesema kwamba toka mwezi January ulipoanza mwaka huu suala la huduma ya maji kwenye maeneo yao imekua ni chamgamoto kubwa kuipata huduma hiyo.

Wamesema ukosefu wa maji umesababisha adha kubwa kwao ambapo baadhi yao hutumia gharama kubwa kununua maji ya dukani kwa mahitaji ya nyumbani na huku wegine wakisema kwamba hutumia muda mwingi kwenda visimani kufuata huduma hiyo hali inayo sababisha kutofanya shughuli za kimaendeleo katika nyumba zao.

Aidha,wananchi hao wameitupia lawama mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira jijini Tanga,(TANGA UWASA) kwa kushindwa kutoa taarifa mapema juu ya changamoto hiyo.


MAJLIS MEDIA imefika katika ofisi za mamlaka hiyo ambapo kwa upande wake mkurugnzi wa mamlaka hiyo Mhandisi.FARLES ARAM amesema kuwa tatizo liliosababisha kutokea kwa hali hiyo ni kukatika katika kwa umeme ambapo imesababisha kutokea tatizo la ghafla kwenye njia kuu ya kupeleka umeme eneo la mtambo wa kutibu maji uliopo MOWE na kusababisha mtambo wa kutibu  na kusukuma maji umesimamisha uzalishaji wa majisafi kutokana na tatizo hilo.



No comments