Kata ya MABOKWENI yakabiliwa na changomoto za elimu.

Shule za msingi KIRUKU,MABOKWENI na KIBAFUTA zilizopo kata ya MABOKWENI jijini TANGA,zinakabiliwa na changamoto mbalimbali za kitaaluma hali inayosababisha wanafunzi kushindwa kupata elimu bora katika shule hizo.

Miongoni mwa changamoto zilizopo katika shule hizo ni uchakavu wa miundombinu ya madarasa ambapo kuna baadhi ya madarasa yameonyesha nyufa kubwa jambo linalohatarisha usalama wa maisha ya wanafunzi na walimu shuleni hapo huku suala la uchache wa miundombinu ya madarasa kwa wanafunzi wa darasa la kwanza likijitokeza hali inayowalazimu wanafunzi kurundikana katika darasa moja na kusababisha usumbufu mkubwa kwa walimu wakati wa ufundishaji.

Aidha,mbali na changamoto hizo pia shule hizo zinakabiliwa na tatizo la uchache wa matundu ya vyoo,ukosefu wa milango kwa baadhi ya madarasa,uchakavu wa nyumba za walimu wakuu sambamba na ukosefu wa ofisi za walimu kwa baadhi ya shule hizo.

Hayo yamebainishwa hii leo na mwanahabari mwandamizi wa  MAJLIS MEDIA alipofanya ziara ya kuzitembelea shule hizo kwa lengo la kujionea hali ya mwitikio wa wanafunzi kipindi hiki cha mwezi January katika kata hiyo ya Mabokweni jijini Tanga.

Mwanahabari huyo mwandamizi wa MAJLIS MEDIA amemtafuta Diwani wa kata hiyo ya MABOKWENI kupitia tiketi ya chama cha wananchi CUF,Mheshimiwa JUMA RAMADHANI ,ambapo kwa upande wake amesema kuwa changamoto hizo zipo kwa muda mrefu lakini hakuna hatua za awali zilizochukuliwa kutoka kwa viongozi husika wa halmashauri ya jiji la TANGA juu ya kutafuta utatuzi wa changamto hizo kwenye shuel hizo.

Aidha,ametumia nafasi hii kwa kumuomba mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya jiji la Tanga,Bwana DAUDI MAYEJI kuweka bajeti ili kuzitatua changamoto hizo.

Katika hatua nyengine MAJLIS MEDIA ilipotaka kuzungumza na walimu wa shule hizo kwa upande wao waligoma kuzungumza chochote hadi hapo watakapopata kibali maalumu kutoka kwa mwajiri wao ambae ni mkurugenzi wa jiji la Tanga DAUDI MAYAJI huku MAJLIS MEDIA ikifanya jitihada za makusudi za kumpata mkurugenzi wa jiji la Tanga ama afisa elimu wilaya ili aweze kuzizungumzia changamoto hizo na kujua hatima ya ufumbuzi wake katika shule hizo.

Awali MAJLISI MEDIA imejionea hali ya uandikishwaji wa wanafunzi wa darasa la kwanza katika shule hizo ambapo hadi sasa katika shule ya msingi MABOKWENI imekwishaandikisha wanafunzi 99 wa darasa la kwanza ambako wanaume 52,wanawake 47 ,shule ya KIRUKU imeandikisha wanafunzi 27 ,wanaume 21 na wanawake 6 na shule ya msingi KIBAFUTA imeandikisha wanafunzi 50,wanaume 30 na wanwake 20.

No comments