Mbowe akerwa na lowasa,atema cheche

Muda mfupi baada ya Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Edward Lowassa kukutana na kufanya mazungumzi na Rais Dkt John Pombe Magufuli na kusifu utawala wake, Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe amezungumza na kusema kuwa, kauli iliyotolewa na Lowassa wakati wa ziara yake ya Ikulu leo, sio msimamo cha chama hicho.
Lowassa ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, amekutana na Rais Dkt Magufuli Ikulu na kumsifu kwa namna anavyoiongoza nchi pamoja na kutekeleza miradi mikubwa ikiwemo ujenzi wa reli ya kisasa (SGR), mradi mkubwa wa kufua umeme wa Strigler’s Gorge ambayo kwa pamoja itaongeza ajira kwa wananchi.
Mbowe akizungumza na Radio Deutsche Welle (DW amesema kuwa huo sio msimamo wa chama chao, kwa sababu wao hunafanya maamuzi kupitia vikao, na hutoa maazimio ya pamoja baada ya kutafakari na kujadiliana kwa upana wake kila hoja.

Aidha, Mbowe ametaja matukio mbalimbali yanayopelekea kukandamiza demokrasia nchini, watu kupotea na wengi kuokotwa wakiwa wamekufa, huku uchumi pia ukikidima na kuhoji mtu anatoa wapi ujasiri wa kupongeza serikali ya awamu ya tano, chini ya Rais Dkt John Pombe Magufuli.

No comments