Serikali yaombwa kuruhus uchimbaji madini

Wachimbaji wadogo wadogo wa madini mkoani Tanga, wameiomba serikali kuruhusu maeneo yenye madini kuchimbwa ili wananchi waweze kujipatia kipato na kuendelea kiuchumi.

Wakizungumza na MAJLIS MEDIA, mapema leo hii, wachimbaji hao wadogo wamesema tanga ni miongoni mwa mikoa yenye ardhi iliyo na madini lakini bado yamezuiwa kutochimbwa tangu kugundulika na kusababisha hali ya uchumi kwa wananchi kupungua kwa kiasi kikubwa.

Wakizungumza kwa hisia kali wachimbaji hao wamemwomba waziri mwenye dhamana wa wizara ya madini kufuatilia maeneo yote katika wilaya tofauti mkoani hapa ili kuruhusu wachimbaji kuchimba madini hayo kwa kufuata utaratibu wa kisheria.

Aidha wamesema kuna maeneo ambayo hayawezi kuleta athari yeyote kimazingira lakini wanashangaa kuona wamezuiliwa kuchimba jambo ambalo linawakatisha tamaa katika kupiga hatua za kimaendeleo.

Wameongeza kuwa mikoa mingi ya bara inagundulika migodi kila wakati lakini viongozi husimamia na kuruhusu wachimbaji wadogo kuendelea na shughuli za uchimbaji tofauti na mkoa wa Tanga ambapo maeneo mengi yaliyojitokeza madini yamezuiliwa mpaka muda huu ukiachilia mbali yale yaliyopo katika vyanzo vya maji na misitu ya hifadhi.





No comments