Wazazi wilayani Lushoto wawaamuru watoto kujaza majibu ya uongo mtihan darasa la7
Baadhi ya wazazi wilayani LUSHOTO mkoani
TANGA,wametajwa kuwa ni chanzo cha kufeli kwa baadhi ya wanafunzi wa darasa la
saba kwa kuwaamuru kujaza majibu ambayo si sahihi katika mitihani ya taifa kwa
lengo la kukwepa mahitaji ya shule pindi watoto wao wanapopaswa kujiunga na
kidato cha kwanza.
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya
Lushoto KAZIMBAYA MAKWEGA ameyasema hayo hiii leo wakati alipokua akizungumza kwa
njia ya simu na mwanahabari wa MAJLIS MEDIA.
KAZIMBAYA amesema kwa kipindi cha mwaka
jana hali hiyo ilishamiri katika halmashauri yake jambo ambalo amesema
lilishusha kwa kiasi fulani hali ya ufaulu wa wanafunzi wa darasa la saba ambapo
ametoa onyo kali kwa wazazi kuacha mara moja mchezo huo.
Aidha,katika
hatua nyengine mkurugenzi huyo ameizungumzia hali ya mwitikio wa wazazi
kuwapeleka watoto wao kujiunga na darasa la awali ambapo amesema kwa mwaka huu
mwitikio ni mkubwa kuliko mwaka jana katika kipindi hiki cha mwezi January.
Mkurugenzi
KAZIMBAYA amesema kwa sasa shule nyingi za msingi katika hamashauri yake zina
changamoto ya miundombinu ya madarasa hali inayowalazimu baadhi ya wanafunzi
kurundikana kwa wingi kwenye madarasani.
Post a Comment