Wajawazito na wazaz Bombo walia na wahudumu

Baadhi ya wahudumu wa afya katika hospital ya rufaa ya mkoa wa TANGA BOMBO,bado wanaendelea kulalamikiwa na wananchi kutokana na tabia yao ya utoaji lugha zisizokua na staha kwa wagonjwa hospitalini hapo.

Wakizungumza na MAJLIS MEDIA hii leo baadhi ya wagonjwa na wananchi hospitalini hapo wamesema kwamba licha ya rais wa jamuhuri wa muungano wa Tanzania Dkt JOHN POMBE MAGUFUL kujitahidi kuleta nidhamu kwa watumishi wa umma kwa kukemea vikali wafanyakazi wazembe na wanaokiuka sheria na kanuni za utumishi bora wa kazi za umma kwa kuwanyanyasa wananchi bado tatizo hilo linaendelea kwa baadhi ya wafanyakazi wa afya katika hospita hiyo.

Aidha,wamesema kwamba miongoni mwa hodi iliyotawaliwa na vitendo hivyo kwa baadhi ya wahudumu wa afya hospitalini hapo ni hodi ya wajawazito na uzazi.

Awali mwanahabari mwandamizi wa MAJLIS MEDIA amefanya ziara hospitalini hapo na kushuhudia baadhi ya wagonjwa wakinung’unika kwa ishara ya kutoridhishwa na huduma za hospital hiyo ambapo kwa sauti ya juu mgonjwa mmoja alisikika akisema kwamba ‘‘ni mara mia moja ukatibiwa hospitali binafsi kwenye gharama kubwa kuliko kung’ang’ania hospitali hiyo ya  serikali’’ ambapo alikua akimaanisha kuwa huduma inayotolewa hospitalini hapo sio bora ukilinganbisha na hospitali binafsi.

Katika hatua nyengine wananchi na wagonjwa waliofika hospitalini hapo wamelalamikia suala la gharama za matibabu kuwa juu katika hospitali hiyo kuliko ubora wa matibabu yenyewe ambapo wamedai kuwa asilimia kubwa za dawa muhimu za mgonjwa wanazoandikiwa na madaktari wanaambiwa wakanunue kwenye maduka ya dawa binafsi.

Ikumbukwe kuwa mwishoni mwa mwaka jana mganga mkuu wa mkoa wa TANGA,Dkt ASHA MAHITA alizungumza na MAJLIS MEDIA kwa kusema kuwa anaendelea kupokea kero mbalimbali za wananchi juu ya namna ya kuboresha huduma za afya katika hospital ya rufaa ya mkoa wa Tanga Bombo kupitia sanduku la maoni hospitalini  hapo ama wananchi kufika ofisini kwake katika jengo la mkuu wa mkoa wa Tanga ili wananchi waweze kupatiwa huduma stahiki ya afya katika hospita hiyo.


No comments