Wapitishaj unga jijin tanga kukiona cha moto.


TANGA.
Kamanda wa jeshi la polis mkoa wa  TANGA, kamishina msaidizi mwandamizi wa jeshi,SACP EDUARD BUKOMBE,ameahidi kulidhiibiti wimbi la biashara ya madawa ya kulevya maeneo mbalimbali mkoani hapa.

Kamanda BUKOMBE amesema dhamira hiyo imejiri kutokana na maeneo mengi mkoani hapa kubainika uwepo wa kero nyingi za matumizi ya madawa ya kulevya ikiwemo mirungi,bangi sanjari na madawa ya kulevya ya viwandani ambako amesema Jambo hilo hatolifumbia macho kamwe katika nafasi yake.
Aidha,amesema kuwa suala hilo tayali wamekwishalianza huku akiwaomba wananchi kutoa taarifa ofisini kwake pindi wanapobaini uwepo wa watu wachache wanaojihusisha na suala hilo ili jopo la askari wake waweze kuchukua hatua stahiki.

Awali amesema kwamba changamoto iliopo katika suala hilo ni uwepo wa njia nyingi za panya za usafirishaji wa madawa hayo katika mkoa ambapo amesema hivi saa wamejipanga kikamilifu kudhibiiti njia zote hizo ikiwa kwa upande wa baharini.

RPC.BUKOMBE amesema zoezi hilo linakwenda sambamba na suala la kuwahimiza madereva kufuata sheria za usalama barabarani kwa kuwa kuna baadhi yao wanakiuka sheria hizo kwa makusudi.

Hayo ameyasema hii leo ofisini kwake wakati alipokua akifanyiwa mahujiano mahsusi na mwanahabari wa MAJLIS MEDIA kuhusu hali ya ulinzi na usalama kimkoa.

Amesema kuhusu hali ya ulinzi na usalama katika mkoa amesema ipo shwari licha ya uwepo wa wachache wanaoleta usumbufu lakini suala la kutii sheria bila shuruti na kuongeza kwamba tayari amekwishaagiza vijana wake kuendelea na doria mbalimbali kuwabaini watu hao ili wachukuliwe hatua kali za kisheria ikiwa ni kufikishwa mahakamani.


No comments