ASKARI WALA RUSHWA TANGA KUKIONA CHA MTAMA KUNI

TANGA.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa TANGA, kamishina msaidizi mwandamizi wa Jeshi la Polisi EDUARD BUKOMBE amewataka wananchi kuwafichua askari Polisi wanaojiusisha na vitendo vya rushwa huku akitoa rai kwa askari wenye mchezo huo kujitathimini upya kama wanastahili  kuwa wahudumu wa jeshi hilo.

Kamanda BUKOMBE ametoa kauli hiyo ofisini kwake  wakati alipokua akifanyiwa mahujiano mahsusi na  MAJLIS MEDIA  ambapo amesema kanuni na sheria za utumishi haziruhusu mtumishi wa umma  kujiusisha na vitendo vya rushwa na kusema katika nafasi yake hatoweza kumvumilia mtumishi wa Jeshi hilo anaejiusisha na vitendo hivyo.

Aidha amewataka wananchi kutoa taarifa za viashiria vya uvunjifu wa amani katika maeneo yao huku akitaja mipango mikakati ya Jeshi lake ni kuwa karibu zaidi na wananchi ili suala la ulinzi na usalama liwe ni la kila mtanzania na si Jeshi la Polisi pekee.

Hata hivyo amesema wameanzaa doria katika maeneo ya bahari kwa lengo la kutokomeza biashara za magendo huku akisema matukio ya uingizwaji na ukamataji wa madawa ya kulevya yamepungua kwa kiasi kikubwa.


No comments