Serikali mkoani TANGA yatumia zaidi ya Bilioni 30.
Serikali mkoani TANGA,imetumia
Bilioni 30,416,058,340.92 katika utekelezaji wa mpango wa kunusuru kaya masikini
nchini TASAF III kwa walengwa 55,703 wa mpango huo mkoani hapa.
Katibu tawala mkoa wa
TANGA,Mhandisi.ZENA SAID ameyasema hayo alipokua akizungumza na MAJLIS MEDIA
ofisini kwake.
Awali Mhandisi.ZENA amesema
kwamba katika mkoa wa Tanga,utekelezaji wa mpango huo uliziduliwa rasmi mkoani
hapa toka mwezi November mwaka 2014 na kutekelezwa katika vijiji na mitaa 681
yenye kaya 61,437,na kusema kutokana na vifo,kuhama kwa walengwa na uwepo wa
kaya zisizokidhi vigezo vya kuwa walengwa ndani ya mpango,baadhi ya kaya
ziliondolewa kwenye orodha ya walengwa wa mpango,hivyo hadi kufikia mwezi Noveber,2017
mpango ulikua na jumla ya walengwa 55,703 katika mkoa wa Tanga.
Aidha,katibu tawala huyo
mkoa wa Tanga,amesema miongoni mwa halmashauri zilizojumulishwa na kupata mgao
huo ni Tanga jiji yenye vijiji/mitaa 88,kaya 5321 ambako ilipatiwa kiasi cha
fedha za mpango huo 2,870,712,500,Muheza yenye vijij/mitaa 90,kaya 7592 na
kupatiwa fedha 3,552,132,954.55,Mkinga yenye vijiji/mitaa 57,kaya 4580 na
kupatwa fedha za mgao 2,340,205,318.18,Pangani yenye vijiji/mtaa 35,kaya 3951
na kupatiwa 2,025,450,090.91,Korogwe yenye vijiji/mitaa 80,kaya 7724 na
kupatiwa 3888075272.73,Korogwe mji yenye vijiji/mitaa 24,kaya 2894 na kupatiwa
mgao wa fedha 1,538,769,431.82,Handeni
yenye vijiji/mitaa 54,kaya7264 na kupewa mgao wa fedha 3,860,314,000,Handeni
mij yenye vijiji/mitaa 40,kaya 2982 na kupatiwa mgao wa fedha 1,555,627,204.55.
Lushoto na bumbuli
vijiji/mtaa146,kaya 6784 na kupatiwa fedha za mgao 5,072,554,886.36 pamoja na
Kilindi yenye vijiji/mitaa 67,kaya 6611 na kupatiwa fedha za mgao
3,713,216,681.82 ambapo kwa mgawanyo huo ndio umefainiksha kupatikana jumla ya
vijij/mitaa 681,kaya 55,703 sambamba na fedha Bilioni 30,416,058,340.92 za
utekelezaji wa mpango wa TASAF III katika mkoa mzima wa Tanga.
Awali,ametaja mafanikio yaliopatikana
kutokana na mpango huo kuwa ni vikundi vya kuweka Akiba na kuwekeza vimenufaika
kutokana na elimu ya kuwek akiba na kuwekeza inayoendelea kutolewa na timu ya
uwezeshaji ya sekretari ya mkoa kwa kushirikiana na wasimamizi wa mpango katika
maeneo yautekelezaji wa kuanzia ngazi ya halmashauri.Kuanzishwa kwa vikundi vya
kuweka na kukopa kutokana na kuanzishwa kashughuli za kiuchumi za ufugaji,mama
lishe,kilimo chambogamboga ambazo zimewezesha kuundwa kwa vikundo vya kuweka na
kukopa na kuwaongeezea kipato na kuboresha maisha ya walengwa na kuweza
kujiwekea akiba.
Pia amessema kaya masikini
zimeanza kuwa na uhakika wa kujikimu katika maisha yao ya kila siku na kunza
kujiwekea akiba kupitia mpngo wa miradi ya kutoa Ajira ya muda wa TASAF III,Kutokana
na kutolewa ruzuku ya masharti ya elimu, watoto kutoka kaya masikini wameweza
kuhudhuria shule vizuri na kuongeza ufaulu katika masomo hivyo kuinua taaluma,Kupunguza
idadi ya watoto wasiojua kusoma na kuandika ambao wengi wao hutoka katika kaya
masikini,Kupungua kwa vifo kwa kina mama wajawazito,watoto chini ya miaka
mitano na wazee kutokana na makundi hayo kupata huduma muhimu za afya kwa
wakati kupitia matumizi ya bima ya afya (CHF) sanjari na kujenga uwezo wa
wananchi kutoka kaya masikini kushiriki vikao mbalimbali vya matumizi katika
ngazi za msingi.
Halikadhalika ameelezea
changamoto zinazoukabili mpango huo ambapo ni Uwepo wa kaya nyingi masikini
ambazo hazijafikiwa na mpango huo kutokana na upungufu wa wa rasilimali fedha,Baadhi
ya walengwa wa mpango kufutwa kimakosa kwenye orodha ya malipo bila ya maelezo
hivyo kukosa haki ya kupata fedha za kujikimu pamoja na walengwa wengi wa
mpango huo hasa katika maeneo ya vijijini wazee wasio na uwezo wa kutumika
(nguvu kazi) katika uzalishaji ,hivyo ruzuku wanazopatiwa ni kwa ajili ya
chakula na sio kujiongezea kipato kwa njia ya kuwekeza katika miradi ya
kiuchumi.
Mhandisi ZENA SAIDI amesema
kuwa serikali ya mkoa wa Tanga itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali
ndani ama nje ya mkoa ili kuhakikisha kwamba malengo ya TSAF III kuzinusuru
kaya masikini yanafikiwa.
Post a Comment